THBUB yawafikia zaidi ya wananchi 89,000 kupitia elimu ya haki za binadamu
Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imeendelea kuimarisha uelewa wa wananchi kuhusu haki za binadamu na misingi ya utawala bora kwa kuwafikia zaidi ya wananchi 89,000 kupitia njia mbalimbali za utoaji elimu katika mwaka wa fedha 2025/2026. Elimu hiyo ilitolewa kupitia mafunzo kwa makundi mbalimbali ya jamii, vipindi vya redio na televisheni, mitandao ya kijamii, huduma ya ujumbe mfupi wa simu (Bulk SMS) pamoja na usambazaji wa vipeperushi na machapisho ya elimu. Taarifa hiyo imetolewa na Msemaji wa Tume hiyo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Elimu kwa Umma, Mawasiliano,Utafiti na Nyaraka wakati akiongea na vyombo vya habari katika viwanja vya Maonesho ya Kimataifa ya Biashara saba saba leo Juni 29,2029 Bi. Mnanka amesema katika kipindi hicho, wananchi zaidi ya 80,000 walifikishiwa ujumbe wa elimu kupitia simu za mkononi, huku vipeperushi 39,129 na vitabu 200 vya elimu vikisambazwa kwa wananchi ili kuongeza uelewa kuhusu haki za binadamu, utawala bora na namna ya kuwasilisha mala...